Monday, April 15, 2013

MAN CITY YAFUZU FAINALI YA F.A CUP

      CHELSEA-1 MANCHESTER CITY-2
                                                
Samir Nasri mapema kipindi cha kwanza aliipatia Man City bao la kuongoza baada ya kutokea piga nikupige golini mwa Chelsea hali ilotokana na kazi nzuri ya kiungo wa City,Yaya Habib Toure kupandisha shambulizi nzuri hadi mapumziko City walikuwa mbele kwa goli moja.
 Aguero huyu akiwa na saikolojia nzuri baada ya kuwafunga goli zuri mahasimu wao Man utd wiki ilopita kwenye mechi ya ligi tena aliwapeleka kati Chelsea na kufanya matokeo kuwa mbili bila,baadaye mshambuliaji wa kimataifa wa Senegali Demba Ba aliwafungia Chelsea goli la kufutia machozi ambapo matokeo yalibaki vivyo hivyo hadi filimbi ya mwisho inalia.

No comments:

Post a Comment