Monday, April 15, 2013

MAN UTD AJIKITA ZAIDI KILELENI MWA LIGI KUU ENGLAND


 Mpaka filimbi ya mwisho inapulizwa MAN UTD alikuwa mbele kwa bao mbili hali inayofanya timu hiyo yenye maskani katika jiji la Manchester kuzidi kuweka matumaini ya kuchukua ubingwa wa ishirini wa ligi kuu ya Uingereza chini ya kocha Sir Alex Fergusson,alikuwa ni Michael Carrick mapema katika kipindi cha kwanza na baadaye hakunaga Van magoli,mdachi Robin Van Persie aliyeshindilia msumali wa penati baada ya kukwatuliwa ndani ya eneo la hatari.
                                   


                                                

Pengine kilichovutia zaidi ndani ya mchezo ilikuwa baada ya dakika ya 76 Van persie kufunga bao la penati na hivyo kukata ukame wa mabao ulokuwa umemuandama karbia miezi miwili na kufikisha magoli ishirini nyuma ya kinara wa ufunga Luis Suares na kushangilia kwa nguvu kwa kumkumbatia kocha wake Alex Fergusson

                   

                                  

No comments:

Post a Comment