Wednesday, April 17, 2013
Tz ya kijanja: MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 66/-Mechi ya Lig...
Tz ya kijanja: MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 66/-Mechi ya Lig...: MECHI YA AZAM, SIMBA YAINGIZA MIL 66/- Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa jana (Aprili 14 mwaka huu) Uw...
BREAKING NEWZ;BI KIDUDE AFARIKI
R.I.P BI FATUMA BINTI BARAKA
BREAKING NEWS: R.I.P Bi.Kidude
BREAKING NEWS: R.I.P Bi.Kidude
Msanii nguli wa Muziki wa Taarab asili kutokea visiwa vya Zanzibar
nchini Tanzania, Fatuma binti Baraka maarufu kama Bi. Kidude amefariki
dunia leo huko Zanzibar.
Monday, April 15, 2013
SIMBA,AZAM HAKUNA MBABE TAIFA
SIMBA-2 AZAM-2
Ndoto ya Azam kuisogelea Yanga kileleni imeingia doa jana baada
ya kulazimishwa sare 2-2 na Simba iliyoundwa na wachezaji chipukizi
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabingwa watetezi Simba walikuwa wa kwanza kupata
mabao yao mawili kupitia mshambuliaji wao Ramadhani Singano kabla ya
Azam kuamka na kusawazisha mabao kupitia penalti ya Kipre Tchetche na
bao lililofungwa na Humpfrey Mieno.
Kwa matokeo hayo Azam imefikisha pointi 47, wakati
Yanga wakiwa kileleni na pointi 52, huku Simba wakibaki nafasi ya nne
na pointi zao 36 na kupoteza matumaini ya kuiwakilisha nchi katika
mashindano ya kimataifa mwakani.
Katika mechi ya jana, Azam
walianza mpira vizuri na kufanikiwa kufika langoni mwa Simba katika
dakika ya kwanza baada ya shuti la John Bocco kutoka pembeni kidogo ya
goli.
Simba walianza vizuri jibu mapigo baada
ya mpira wa kona iliyopigwa na Mrisho Ngassa kutua kichwani mwa Shomari
Kapombe, lakini kipa wa Azam, Mwadini Ally alikuwa makini kuokoa hatari
hiyo.
Chipukizi Singano aliwainua mashabiki wa Simba kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 11 akimalizia kazi nzuri ya Ngassa.
Wakati Azam wakiwa hawaamini kinachotokea Singano
alifunga bao la pili katika dakika ya 18, baada ya Ngassa kumtoka beki
wa Azam, David Mwantika na kupitisha pasi nzuri kwa chipukizi huyo.
Beki wa Azam, Mwantika alionekana mzito na
kushindwa kwenda na kasi ya Ngassa na Singano waliomgeuza walivyotaka na
kuipa Simba mabao mawili ya haraka.
Baada ya bao hilo kocha wa Azam, Stewart Hall
alimtoa Luckson Kakolaki na kumwingiza Hamis Mcha katika dakika ya 20.
Winga huyo alitumia dakika nane tu kabla ya kuangushwa kwenye eneo la
hatari na beki Miraj Mdigo na mwamuzi Oden Mbaga kutoa penalti
iliyofungwa na Kipre Tchetche.
Kiungo wa kimataifa wa Kenya, Humpfrey Mieno
aliisawazishia Azam bao katika dakika ya 71 akiunganisha vizuri mpira wa
adhabu uliopigwa na Mcha baada ya Tchetche kufanyiwa madhambi na Said
Nasoro Cholo.
Katika mechi hiyo, mwamuzi Mbaga alimtoa katika benchi, Kocha Hall na kumtaka aende kukaa jukwaani baada ya kumbwatukia akipinga uamuzi wake
MAN CITY YAFUZU FAINALI YA F.A CUP
CHELSEA-1 MANCHESTER CITY-2
Samir Nasri mapema kipindi cha kwanza aliipatia Man City bao la kuongoza baada ya kutokea piga nikupige golini mwa Chelsea hali ilotokana na kazi nzuri ya kiungo wa City,Yaya Habib Toure kupandisha shambulizi nzuri hadi mapumziko City walikuwa mbele kwa goli moja.
Aguero huyu akiwa na saikolojia nzuri baada ya kuwafunga goli zuri mahasimu wao Man utd wiki ilopita kwenye mechi ya ligi tena aliwapeleka kati Chelsea na kufanya matokeo kuwa mbili bila,baadaye mshambuliaji wa kimataifa wa Senegali Demba Ba aliwafungia Chelsea goli la kufutia machozi ambapo matokeo yalibaki vivyo hivyo hadi filimbi ya mwisho inalia.
Samir Nasri mapema kipindi cha kwanza aliipatia Man City bao la kuongoza baada ya kutokea piga nikupige golini mwa Chelsea hali ilotokana na kazi nzuri ya kiungo wa City,Yaya Habib Toure kupandisha shambulizi nzuri hadi mapumziko City walikuwa mbele kwa goli moja.
Aguero huyu akiwa na saikolojia nzuri baada ya kuwafunga goli zuri mahasimu wao Man utd wiki ilopita kwenye mechi ya ligi tena aliwapeleka kati Chelsea na kufanya matokeo kuwa mbili bila,baadaye mshambuliaji wa kimataifa wa Senegali Demba Ba aliwafungia Chelsea goli la kufutia machozi ambapo matokeo yalibaki vivyo hivyo hadi filimbi ya mwisho inalia.
MAN UTD AJIKITA ZAIDI KILELENI MWA LIGI KUU ENGLAND
Mpaka filimbi ya mwisho inapulizwa MAN UTD alikuwa mbele kwa bao mbili hali inayofanya timu hiyo yenye maskani katika jiji la Manchester kuzidi kuweka matumaini ya kuchukua ubingwa wa ishirini wa ligi kuu ya Uingereza chini ya kocha Sir Alex Fergusson,alikuwa ni Michael Carrick mapema katika kipindi cha kwanza na baadaye hakunaga Van magoli,mdachi Robin Van Persie aliyeshindilia msumali wa penati baada ya kukwatuliwa ndani ya eneo la hatari.
Pengine kilichovutia zaidi ndani ya mchezo ilikuwa baada ya dakika ya 76 Van persie kufunga bao la penati na hivyo kukata ukame wa mabao ulokuwa umemuandama karbia miezi miwili na kufikisha magoli ishirini nyuma ya kinara wa ufunga Luis Suares na kushangilia kwa nguvu kwa kumkumbatia kocha wake Alex Fergusson
MWANAMKE AL;IYEDAIWA KUFARIKI MIAKA MITANO ILOPITA AFUFUKA
MWANAMKE ALIYEDAIWA KUFARIKI MIAKA MITANO ILOPITA AFUFUKA
Mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita Afufuka
Mwanamke anayedaiwa kufariki miaka mitano iliyopita Afufuka
MJI wa Geita na maeneo ya jirani juzi ulikumbwa na taharuki ya aina
yake, pale mwanamke ambaye anadaiwa kwamba alifariki miaka mitano
iliyopita alipoonekana akiwa hai katika eneo la Kasamwa. Inadaiwa kwamba
Flora Onesmo (45) alifariki Februari 28, 2008 katika Hospitali ya
Wilaya ya Geita na kuzikwa katika Kijiji cha Nakasenya, Kata ya
Butundwe, lakini juzi alfajiri alikutwa ameketi nje ya nyumba ya dada
yake aitwaye Monica James, anayeishi Kasamwa.
Aliyekuwa wa
kwanza kumwona Flora ni mdogo wake aitwaye Monica Onesmo ambaye baada ya
kuamka saa 11:00 alfajiri nyumbani kwa dada yake, alimwona mwanamke
aliyekuwa ameketi nje ya nyumba hiyo, lakini alimfananisha mwanamama
huyo na marehemu dada yake.
“Baada
ya kumwona nilimwita mtoto wake tunayekaa naye na nikampigia simu dada
(Monica) ambaye alikuwa amelala chumba kingine nikamwambia kwamba
nimeamka na kumkuta mwanamke amekaa hapa nje, lakini kila nikimwangalia
anafanana na marehemu dada yetu,” alisema Jubili na kuongeza kwamba
alipowaita wote walitoka nje.
Alisema mtoto wa Flora (marehemu
anayedaiwa kufufuka) anaitwa Rebeka Elisha (16) na kwamba walimchukua
tangu 2008 wakati mama yake huyo alipofariki dunia katika Hospitali ya
Geita ambako alikuwa amelazwa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa ini.
Rebeka ambaye ni mtoto wa nne wa Flora alisema: “Mama mdogo alituita
sisi tulikuwa tumelala akasema kwamba nje kuna mwanamke ambaye anafanana
na marehemu mama yetu, ndipo na sisi tukatoka na kweli kumwangalia
alikuwa ni yeye kabisa.”
Alisema walipomuhoji mama yake huyo
kwamba ametokea wapi, aliwaeleza kuwa ametoka eneo la Katoro kwa mganga
na aliletwa na watu ambao hakuwatambua Alhamisi saa 1:30 usiku ndani ya
gari na watu hao walimshusha kwa mtu aitwaye Juma Luchunga ambaye ni
jirani na dada zake hao.
Kauli ya Flora
Akizungumza na
waandishi wa habari, Flora alisema yeye ni mkazi wa Katoro na kwamba
alitokea Katoro nyumbani kwa mganga wa jadi ambaye hata hivyo hakumtaja
kwa maelezo kwamba wataalamu wake (majini) wamemkataza.
“Nilikuwa
naishi kwa mganga wa kienyeji ila alikuja mwanaume wakati nikiwa pale
akaninywesha dawa kisha tukapakizwa kwenye gari na watu wawili ambao
sikuwatambua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume mpaka hapa Kasamwa
tukashushwa saa 1:00 jioni,”alisema Flora.
Alisema alipofika
Kasamwa alikwenda kunywa uji kwa mama mmoja ambaye pia hakumtaja na
kwamba baadaye alipelekwa nyumbani kwa mtu mwingine saa nne usiku,
lakini watu wa nyumba hiyo walipomwona walimwambia: “Hapa si kwako
twende tukupeleke kwa ndugu yako” na ndipo wakampeleka kwa dada yake
ambako aliketi nje hadi alfajiri.
Flora alisema kabla ya kuishi kwa
mganga alikuwa akiishi porini ambako alitupwa na watu asiowafahamu na
baadaye aliokotwa na wasamaria wema ambao ndiyo walimpeleka kwa mganga
ambako alikuwa akiishi muda wote(SOUCE;MWANZA CELEBRITY PAGE)
Saturday, April 13, 2013
YANGA YAZIDI KUTETEA UBINGWA,YAIPIGA OLJORO
YANGA UTAIPENDA TU, YAICHAPA OLJORO 3-0

Young Africans imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri
ya msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom baada kufikisha point 52 bao 40
ya kufunga, pointi 6 mbele ya timu inayoshika nafasi ya pili Azam Fc
yenye pointi 46 huku timu zote zikiwa na michezo sawa 22.
Kikosi
cha mholanzi Ernest Brandts kiliuanza mchezo kwa kasi na katika dakika
ya 5 ya mchzo kupitia kwa mlinzi wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro'
aliipatia bao la kwanza kwa kichwa baada ya kumalizia mpira wa kona
iliyokuw aimepigwa na kiungo Haruna Niyonzima.
Watoto
wa jangwani walionyesha kuwa wamedhamiria kupata ushindi mnono leo
kwani waliweza kucheza soka safi na la kuvutia huku Hamis Kiiza na
Didier Kavumbagu wakikosa mabao ya wazi ndani ya dakika 15 za kwanza.
Kiungo
chipukizi mwenye kasi Saimon Msuva aliipatia Young Africans bao pili
dakika ya 19 ya mchezo kufuatia kuwazidi ujanja walinzi wa timu ya JKT
Olljoro na Msuva kumchambua kwa umaridadi mlinda mlango wa JKT Oljoro na
kuhesabu bao la pili kwa timu ya Yanga.
Yanga
iliendelea kulishambulia lango la JKT Oljoro muda wote wa mchezo na
mashuti ya washambuliaji wa Yanga yalimfanya mlinda mlnago huyo kutibiwa
mara kwa mara kwa kukoa michomo ya washambuliaji wa Yanga.
Dakka
ya 43, mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Hamis Kiiza
aliipatia Yanga bao la tatu kufuatia mpira aliopenyezewa na kiungo Frank
Domayo na Kiiza kuwatoka walinzi wa JKT Oljoro na kuiandikia Yanga bao
la tatu.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza, Young Africans 3 - 0 JKT Oljoro.
Kipindi
cha pili kilianza kwa Yanga kufanya mabadiliko ambapo waliingia Nizar
Khalfani na Said Bahanuzi kuchukua nafasi za Didier Kavumbagu aliyeumia
na Simon Msuva mabadiliko yaliongeza ufundi zaidi na kuutalawa mchezo
kwa kipidndi chote.
Said Bahanuzi alifanyiwa
madhambi wakati akiwa ndani ya eneo la hatari akijandaa kumchambua
mlinda mlango wa JKT Oljoro lakini mwamuzi wa mchezo na mwamuzi wa
pembeni wake hawakujali na kuendelea na mchezo.
Zikiwa
zimebakia dakika tano kabla yakumalizika kwa mchezo, kiungo
mshambuliaji Nizar Khalfani alikosa bao la wazi kufuatia shuti lake
kuokolewa na mlinda mlango wake ambapo mpira huo ulipigwa kona ambayo
haikuzaa matunda.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 3 - 0 JKT Oljoro.

Kocha
mkuu wa Yanga Ernest Brandts amesema anashukuru timu yake kupata kwa
ushindi katika mchezo wa leo, kipindi cha kwanza timu yangu ilicheza kwa
nguvu na kupata mabao ya mapema hali iliyoplekea kipindi cha pili
kucheza soka la burudani.
Timu imekua na
mabadiliko makubwa sana kiuchezaji na leo timu imecheza soka safi la
burudani lililoambatana na ushindi, hii ni zawadi kwa washabiki, wapenzi
wa soka na wanachama wa klabu ya Yanga kuwa njia ya kutwaa ubingwa kwa
sasa ni nyeupe.
Yanga inajiandaa na mchezo dhidi
ya timu ya Mgambo Shooting siku ya jumatano mjini Tanga ambapo timu
itasafiri siku ya jumatatu tayari kwa ajili ya mchezo huo ambao ni
muhimu kwa Yanga ili kuendelea kujiweka vizuri katika nafasi ya kutwaa
Ubingwa kabla ya kumalizika kwa msimu.
Young Africans:
1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul/Shadrack Nsajigwa, 3.David
Luhende, 4.Nadir Haroub'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani , 6.Athuman Idd
'Chuji', 7.Saimon Msuva/Nizar Khalfani, 8.Frank Domayo, 9.Didier
Kavumbagu/Said Bahanuzi,10.Hamis Kiiza, 11.Haruna Niyonzima(SOURCE,YOUNGAFRICANS.CO.TZ)
Subscribe to:
Posts (Atom)